95. The Fig

1
وَالتِّينِ وَالزَّيْتُونِ
Naapa kwa tini na zaituni!
2
وَطُورِ سِينِينَ
Na kwa Mlima wa Sinai!
3
وَهَٰذَا الْبَلَدِ الْأَمِينِ
Na kwa mji huu wenye amani!
4
لَقَدْ خَلَقْنَا الْإِنسَانَ فِي أَحْسَنِ تَقْوِيمٍ
Bila ya shaka tumemuumba mtu kwa umbo lilio bora kabisa.
5
ثُمَّ رَدَدْنَاهُ أَسْفَلَ سَافِلِينَ
Kisha tukamrudisha kuwa chini kuliko walio chini!
6
إِلَّا الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ فَلَهُمْ أَجْرٌ غَيْرُ مَمْنُونٍ
Lakini wale walio amini na wakatenda mema, hao watapata ujira usio kwisha.
7
فَمَا يُكَذِّبُكَ بَعْدُ بِالدِّينِ
Basi ni kipi baadaye kitacho kukukadhibishia malipo?
8
أَلَيْسَ اللَّهُ بِأَحْكَمِ الْحَاكِمِينَ
Kwani Mwenyezi Mungu si muadilifu kuliko mahakimu wote?
CopyRight © 2024 Koran.link All Rights Reserved