93. The Forenoon

1
وَالضُّحَىٰ
Naapa kwa mchana!
2
وَاللَّيْلِ إِذَا سَجَىٰ
Na kwa usiku unapo tanda!
3
مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ
Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.
4
وَلَلْآخِرَةُ خَيْرٌ لَّكَ مِنَ الْأُولَىٰ
Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia.
5
وَلَسَوْفَ يُعْطِيكَ رَبُّكَ فَتَرْضَىٰ
Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.
6
أَلَمْ يَجِدْكَ يَتِيمًا فَآوَىٰ
Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi?
7
وَوَجَدَكَ ضَالًّا فَهَدَىٰ
Na akakukuta umepotea akakuongoa?
8
وَوَجَدَكَ عَائِلًا فَأَغْنَىٰ
Akakukuta mhitaji akakutosheleza?
9
فَأَمَّا الْيَتِيمَ فَلَا تَقْهَرْ
Basi yatima usimwonee!
10
وَأَمَّا السَّائِلَ فَلَا تَنْهَرْ
Na anaye omba au kuuliza usimkaripie!
11
وَأَمَّا بِنِعْمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثْ
Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie.
CopyRight © 2024 Koran.link All Rights Reserved