101. The Striking Hour

1
الْقَارِعَةُ
Inayo gonga!
2
مَا الْقَارِعَةُ
Nini Inayo gonga?
3
وَمَا أَدْرَاكَ مَا الْقَارِعَةُ
Na nini kitacho kujuilisha nini Inayo gonga?
4
يَوْمَ يَكُونُ النَّاسُ كَالْفَرَاشِ الْمَبْثُوثِ
Siku ambayo watu watakuwa kama nondo walio tawanyika;
5
وَتَكُونُ الْجِبَالُ كَالْعِهْنِ الْمَنفُوشِ
Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa!
6
فَأَمَّا مَن ثَقُلَتْ مَوَازِينُهُ
Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito,
7
فَهُوَ فِي عِيشَةٍ رَّاضِيَةٍ
Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza.
8
وَأَمَّا مَنْ خَفَّتْ مَوَازِينُهُ
Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu,
9
فَأُمُّهُ هَاوِيَةٌ
Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya!
10
وَمَا أَدْرَاكَ مَا هِيَهْ
Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo?
11
نَارٌ حَامِيَةٌ
Ni Moto mkali!
CopyRight © 2024 Koran.link All Rights Reserved