أَلَمْ نَشْرَحْ لَكَ صَدْرَكَ
Hatukukunjulia kifua chako?
وَوَضَعْنَا عَنكَ وِزْرَكَ
Na tukakuondolea mzigo wako,
وَرَفَعْنَا لَكَ ذِكْرَكَ
Na tukakunyanyulia utajo wako?
فَإِنَّ مَعَ الْعُسْرِ يُسْرًا
Basi kwa hakika pamoja na uzito upo wepesi,
إِنَّ مَعَ الْعُسْرِ يُسْرًا
Hakika pamoja na uzito upo wepesi.
فَإِذَا فَرَغْتَ فَانصَبْ
Na ukipata faragha, fanya juhudi.
وَإِلَىٰ رَبِّكَ فَارْغَب
Na Mola wako Mlezi ndio mshughulikie.