104. The Slanderer

1
وَيْلٌ لِّكُلِّ هُمَزَةٍ لُّمَزَةٍ
Ole wake kila safihi, msengenyaji!
2
الَّذِي جَمَعَ مَالًا وَعَدَّدَهُ
Aliye kusanya mali na kuyahisabu.
3
يَحْسَبُ أَنَّ مَالَهُ أَخْلَدَهُ
Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele!
4
كَلَّا ۖ لَيُنبَذَنَّ فِي الْحُطَمَةِ
Hasha! Atavurumishwa katika H'ut'ama.
5
وَمَا أَدْرَاكَ مَا الْحُطَمَةُ
Na nani atakujuvya ni nini H'ut'ama?
6
نَارُ اللَّهِ الْمُوقَدَةُ
Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa.
7
الَّتِي تَطَّلِعُ عَلَى الْأَفْئِدَةِ
Ambao unapanda nyoyoni.
8
إِنَّهَا عَلَيْهِم مُّؤْصَدَةٌ
Hakika huo utafungiwa nao
9
فِي عَمَدٍ مُّمَدَّدَةٍ
Kwenye nguzo zilio nyooshwa.
CopyRight © 2024 Koran.link All Rights Reserved