86. The Night-Comer

1
وَالسَّمَاءِ وَالطَّارِقِ
Naapa kwa mbingu na Kinacho kuja usiku!
2
وَمَا أَدْرَاكَ مَا الطَّارِقُ
Na nini kitakacho kujuulisha ni nini hicho Kinacho kuja usiku?
3
النَّجْمُ الثَّاقِبُ
Ni Nyota yenye mwanga mkali.
4
إِن كُلُّ نَفْسٍ لَّمَّا عَلَيْهَا حَافِظٌ
Hapana nafsi ila inayo mwangalizi.
5
فَلْيَنظُرِ الْإِنسَانُ مِمَّ خُلِقَ
Hebu naajitazame mwanaadamu ameumbwa kwa kitu gani?
6
خُلِقَ مِن مَّاءٍ دَافِقٍ
Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa,
7
يَخْرُجُ مِن بَيْنِ الصُّلْبِ وَالتَّرَائِبِ
Yatokayo baina ya mifupa ya mgongo na mbavu.
8
إِنَّهُ عَلَىٰ رَجْعِهِ لَقَادِرٌ
Hakika Yeye ana uweza wa kumrudisha.
9
يَوْمَ تُبْلَى السَّرَائِرُ
Siku zitakapo dhihirishwa siri.
10
فَمَا لَهُ مِن قُوَّةٍ وَلَا نَاصِرٍ
Basi hatakuwa na nguvu wala msaidizi.
11
وَالسَّمَاءِ ذَاتِ الرَّجْعِ
Naapa kwa mbingu yenye marejeo!
12
وَالْأَرْضِ ذَاتِ الصَّدْعِ
Na kwa ardhi inayo pasuka!
13
إِنَّهُ لَقَوْلٌ فَصْلٌ
Hakika hii ni kauli ya kupambanua.
14
وَمَا هُوَ بِالْهَزْلِ
Wala si mzaha.
15
إِنَّهُمْ يَكِيدُونَ كَيْدًا
Hakika wao wanapanga mpango.
16
وَأَكِيدُ كَيْدًا
Na Mimi napanga mpango.
17
فَمَهِّلِ الْكَافِرِينَ أَمْهِلْهُمْ رُوَيْدًا
Basi wape muhula makafiri - wape muhula pole pole.
CopyRight © 2024 Koran.link All Rights Reserved