90. The City

1
لَا أُقْسِمُ بِهَٰذَا الْبَلَدِ
Naapa kwa Mji huu!
2
وَأَنتَ حِلٌّ بِهَٰذَا الْبَلَدِ
Nawe unaukaa Mji huu.
3
وَوَالِدٍ وَمَا وَلَدَ
Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa.
4
لَقَدْ خَلَقْنَا الْإِنسَانَ فِي كَبَدٍ
Hakika tumemuumba mtu katika taabu.
5
أَيَحْسَبُ أَن لَّن يَقْدِرَ عَلَيْهِ أَحَدٌ
Ati anadhani hapana yeyote ataye muweza?
6
يَقُولُ أَهْلَكْتُ مَالًا لُّبَدًا
Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali.
7
أَيَحْسَبُ أَن لَّمْ يَرَهُ أَحَدٌ
Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?
8
أَلَمْ نَجْعَل لَّهُ عَيْنَيْنِ
Kwani hatukumpa macho mawili?
9
وَلِسَانًا وَشَفَتَيْنِ
Na ulimi, na midomo miwili?
10
وَهَدَيْنَاهُ النَّجْدَيْنِ
Na tukambainishia zote njia mbili?
11
فَلَا اقْتَحَمَ الْعَقَبَةَ
Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.
12
وَمَا أَدْرَاكَ مَا الْعَقَبَةُ
Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani?
13
فَكُّ رَقَبَةٍ
Kumkomboa mtumwa;
14
أَوْ إِطْعَامٌ فِي يَوْمٍ ذِي مَسْغَبَةٍ
Au kumlisha siku ya njaa
15
يَتِيمًا ذَا مَقْرَبَةٍ
Yatima aliye jamaa,
16
أَوْ مِسْكِينًا ذَا مَتْرَبَةٍ
Au masikini aliye vumbini.
17
ثُمَّ كَانَ مِنَ الَّذِينَ آمَنُوا وَتَوَاصَوْا بِالصَّبْرِ وَتَوَاصَوْا بِالْمَرْحَمَةِ
Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana.
18
أُولَٰئِكَ أَصْحَابُ الْمَيْمَنَةِ
Hao ndio watu wa kheri wa kuliani.
19
وَالَّذِينَ كَفَرُوا بِآيَاتِنَا هُمْ أَصْحَابُ الْمَشْأَمَةِ
Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni.
20
عَلَيْهِمْ نَارٌ مُّؤْصَدَةٌ
Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande.
CopyRight © 2024 Koran.link All Rights Reserved